Na.Dominic Haule
Mhashamu
HENRY
MCHAMUNGU Askofu Msaidizi wa Jimbo kuu la DAR
ES SALAAM, Amewataka watawa kuishi kwa upendo,unyenyekevu na Msamaha katika Maisha ya jumuiya Ili kazi
ya MUNGU
itendeke vizuri.
Askofu
Mchamungu Amesema hayo katika Misa
Takatifu ya kuweka Nadhiri za Daima kwa Masista wawili wa Shirika la Mabinti wa BIKIRA
MARIA EMMACURATE (DMI), iliyofanyika Parokia ya Mtakatifu MARIA
KIMARA
Mwisho, Jimbo kuu la DAR ES SALAAM.
Amesema
miongoni mwa sifa kubwa za utawa ni kujitoa sadaka kwajili ya wengine na kujishusha na sio kuwa watu malumbano na kutokuelewana ndani ya
jumuiya zao jamboa mbalo alimpendezi MUNGU
na ni kinyume na wito wao.
Aidha
amewakumbusha watawa hao kuishi usafi wa moyo siku zote za Maisha yao ya wito
huo kwani wamejitoa kwajili kanisa na
wamejiweka mbali na malimwengu ambayo
yanaweza kuleta changamoto katika maisha yao.
Amehitimisha
kwa kutoa wito kwa kila mkristo mbatizwa kujitoa kwa ajili ya kuhubiri injili na
kumtagaza YESU KRISTO,kwani
hilo ni jukumu lao msingi na sio badala yake kwaachia mapadre na masista peke
yao.
Pia Amewakumbusha
wazazi na Walezi wasio watu wakuwabebesha majukumu ya kifamilia kwa kuwa hao
wamejitoa Maisha yao kwaajili ya kulitumikia kanisa na Watu wa Mungu.
Post a Comment