0

 


Mhashamu STEPHANO LAMECK MUSOMBA OSA Askofu wa Jimbo Katoliki BAGAMOYO, amewataka Wakristo wakatoliki kuwa makini katika kuisikia Sauti ya Mungu wakiomba msaada wa neema yake ili kuitambua Sauti hiyo na Kuifuata.

Askofu Musomba ametoa Wito huo wakati alitoa Homilia kwenye adhimisho la Misa Takatifu ya utolewaji wa Daraja Takatifu ya Upadre kwa Mashemasi wa 4 ambapo 3 ni wa Jimbo na mmoja ni wa Shirika la Mapendo katika Parokia ya Mtakatifu ANTHONY wa PADUA CHUMBAGENI Kanisa Kuu Jimbo Katoliki TANGA.

Aidha ameongeza kuwa wanapoisikia Sauti ya Mungu na Kuifuata wanakuwa utambulisho wa Kristo hivyo amewahimiza wawe na unyenyekevu na utii kwa yule aliyewaita kumtumikia wakitunza utambulisho huo kwa Mungu na kwa Kanisa lake hapa ulimwenguni kwa kuishi Wito wao na kuwahurumia walionewa na kuvunjika Moyo.

Vilevile amewataka wazazi na Walezi pamoja na Waamini wote kushirikiana katika Malezi ya Mapadre hao ili wadumu katika Wito ulioutambulishonwanYesu katika maisha ya Mwanadamu.

Pamoja na mambo mengine amewataka Waamini wote kuwasaidia Mapadre katika Safari yako ya Wito huku akiwataka kuwalea na kuwatumza kwa sadaka na michango yao pasi na kuwategemea katika kule familia walizotoka kwani wamejitoankwa Bwana na weluwa Mali ya Kanisa la Mungu.

Misa Takatifu imeadhimishwa na Mhashamu STEPHANO LAMECK MUSOMBA OSA Askofu wa Jimbo Katoliki BAGAMOYO akishirikiana na Mhashamu THOMAS JOHN KIANGIO Askofu wa Jimbo katoliki TANGA na imehudhuriwa na Mapadre. Masista, Watawa wakike na wakiume, pamoja na Waamini walei kutoka ndani na nje ya Jimbo la Tanga.

 

Post a Comment

 
Top