0
 
 
 
 
 
 
 
 
Takukuru mkoa wa temeke imewakamata watuhumiwa wawili kwa makosa ya kuomba na kupolea rushwa kinyume na sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa Na. 11,2017 kifungu cha Na.15, maafisa hao ni wa TRA kigamboni na ustawi wa jamii wa mahakama ya mwanzo Buguruni.
Manamo tarehe 15 februari, 2018 Bi. Seire Andrea Akilimali, Afisa ustawi wa jamii wa mahakama ya mwanzo ya Buguruni alifikishwa mahakama ya wilaya ya Temeke na kufunguliwa kesi namba 136/18 kutokana na mtego ulioandaliwa na na TAKUKURU na kukamatwa akiomba rushwa ya Tshs.300,00/= na kupokea kiasi cha Tshs.200,000 ili aweze kumsaidia Mwananchi mmoja ambaye ndugu take alihukumiwa jela miezi minane ili aweze kupata wepesi wa kutumikia kifungu  cha nje.
Pia tarehe 28 February, 2018 Stratton Sylvester Mutayabarwa Afisa wa TRA kigamboni alifikishwa mahakama ya wilaya ya Temeke na kufungukiwa kesi Na.180/18 baada ya kupokea rushwa ya Tshs.300,000/= kutoka kwa wananchi mmoja ambaye ni mmiliki wa bucha ili asimchukulie hatua za kisheria kwa kosa la kufanya biashara bila kufuata sheria za kodi, hata hivyo kesi zote mbili zinasikilizwa na watuhumiwa wote Wapo nje kwa dhamana.
Aidha Takukuru inaemdelea Kuwait had garish wananchi wote kutojihusisha kabisa na vitendo vya rushwa kwani kushawishi, kuimba na kupokea rushwa yote ni makosa chini ya sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa namba 11 ya mwaka 2017 na atakayebainika kukihusisha na vitendo hivyo vya rushwa atachukuliwa hatua za kisheria na pia wananchi watoe taarifa kuhusu vitendo vya rushwa kupitia namba ya bure 113.

Post a Comment

 
Top