0


https://encrypted-tbn0.gstatic.com/images?q=tbn:ANd9GcQE2ZgDL4higpXPSkc7TLMonjz4lQ9Cwnl1MQej4S9XoSXEvwOm



Na.Martin Joseph
Wakuu wa makampuni na taasisi  zilizopo hapa nchini wameombwa kuhuzuli  mikutano pamoja na makongamano ili iwasaidie  kupata  fursa  za kimaendeleo na hata kuendeleza na  kuyainua  kiuchumi makampuni  pamoja na taasisi zao.
Hayo yemesemwa na mwenyekiti  wa taasisi ya  kimataifa ya logistiki na usafirishaji (CILT) GEORGE MAKUKE alipokuwa akitoa taarifa kwa vyomo vya habari kuhusu   mkutano wa kimataifa wa taasisi hiyo unaotalajiwa kufanyika Septemba mwaka huu kisiwani Zanzibar.
Amesema kuwa  mikutano pamoja na makongamano mbalimbali  ni moja kati ya sehemu ambazo zimekuwa zikitengeneza   fursa ikiwemo  mafunzo pamoja ajira kwani  watu mbalimbali wamekuwa wakikutana katika sehemu hizo na kubadilisihana mawazo na hata kujengeana uelewa wa jinsi gani wanaweza wakaziiinua na hata kuzipamaendeleo sekta, kampuni na hata  taasisi zao hivyo basi ni vyema kuzitumia sehemu hizo kama mahali pakujipatia  fursa mbalimbali.
Wakati huo huo nae  mkuu wa chuo cha mabaria hapa nchini Dkt.ERICK MASSAMI  ametoa wito kwa kwa vijana  kujifunza mafuzo ya ubaharia ili kuisaidia nchi  kuongeza mapato ya ndani katika maswala ya usafarishaji wa majini kwani imekuwa ikitumia fedha nyingi  kwa  kuwalipa wasafirishaji ambao wanatoka nje ya nchi hivyo hali hiyo imekua ikipelekea hata kiwango cha  mapato ya nchi kushuka.

Post a Comment

 
Top