0

 


Waamini Wakatoliki wamealikwa kujifungamanisha na Mungu ili kumruhusu Mungu atawale maisha yao.

Hayo yamesemwa na Mhashamu TITUS MDOE Askofu wa Jimbo Katoliki Mtwara wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Jubilei ya Miaka 50 ya Parokia ya Mtakatifu PAUL MAJENGO jimboni MTWARA.

Katika homilia yake Mhashamu Mdoe amewahimiza waamini wa Parokia hiyo kuwa na imani thabiti ili kuweza kumtangaza Mungu popote bila ya woga ikiwa ni pamoja na utii wa kweli unyenyekevu na matumaini kwa Mungu aliye Baba wa haki na upendo. 

Kadharika amewasisitiza waamini hao kufuata mfano wa mama BIKIRA MARIA kwa kuonesha upendo kwa jirani na kuwahudumia wa hitaji kwa haraka kwa kufanya hivyo ni kuiishi imani kwa matendo.

Wakati huohuo mara baada ya Adhimisho la Misa Takatifu Mhashamu Mdoe akizungumza na waandishi wa habari amewashukuru waamini kutenda matendo ya huruma na huduma hasa kipindi hiki cha Jubilei na kuwa watu wa shukrani kwa Mungu na wanadamu. 

 

Next
This is the most recent post.
Previous
Older Post

Post a Comment

 
Top