0
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjPhL0Ivx_VeogYe11zUN0W2CR9e52RrltrgoOlxOzNcRXj3x0WQfx28LIaEWrcRl7Q77SVCYcBNdWfnc4RLdI1iuqfpMzs15zrX1Ywq-mkAcktqP2MtQNAK5pljICR_9DQK0lalde3JuDC/s640/MAPOLISI+NJE.jpg
Na.Martin Joseph
 Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro leo amemuapisha Kamishna wa Polisi CP Mohamed Hassan Haji kuwa Kamishna wa Polisi Zanzibar baada ya kuteuliwa na Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania na amiri jeshi mkuu Dkt John Pombe Magufuli

Hafla hiyo ya kuapishwa Kamishna wa Polisi Zanzibar CP Haji imefanyika Makao Makuu ya Jeshi la Polisi jijini Dar es salaam na kuhudhuriwa na makamishina na maofisa wakuu waandamizi wa jeshi la polisi kutoka Tanzania bara na Zanzibar.

Kufuatia kiapo cha utii mbele ya Inspekta Jenerali wa Jeshi la polisi Kamishna wa Polisi Zanzibar CP Mohamed Hassan Haji amesema vipaumbele vilivyotolewa na viongozi wa juu pamoja na maelekezo yote atahakikisha anayashughulikia kwa wakati ili watanzania waishi kwa amani.

Nae Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro amesema,vyombo vya ulinzi na usalama vinashirikiana kwa amani na huku akieleza kuwa  Zanzibar changamoto pekee iliyobaki ni ajali za barabarani na hivyo watahakikisha wanakabiliana na wavunjifu wa kanuni na sheria za barabarani.

Ikumbukwe kuwa CP Mohamed Hassan Haji alijiunga na Peshi la Polisi mwaka 1991 na kupandishwa vyeo mbalimbali ikiwemo Mkaguzi wa Polisi,Mrakibu Msaidizi wa Polisi,Mrakibu wa Polisi,Mrakibu Mwandamizi wa Polisi,Kamishna msaidizi wa Polisi hadi Kamishna wa Polisi na kuteuliwa kuwa Kamishna wa Polisi Zanzibar.

Post a Comment

 
Top