0



                                                              
     https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhu4EuZO9S_o7iufz5FLMkwxs4pOmbxrVra_kWjxepbQKCMoYf_6-sRZJWiBlzW7k2xGIJai8ERGzHF6aG917fdzR-GcR8sLQlkx8mr78Tte5slDYLcnNf5Uj3IsxSi3Ma8VwljI6sEHeY/s1600/1.jpg



 Na.Martin Joseph
Raisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh, Dkt.JOHN POMBE MAGUFULI amemtengua aliyekua mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya BUTIAMA Bw.SOLOMON NGILIULE kwa kinachosadikiwa kuwa ameshindwa kusimamia ipasavyo maeneo yake ya kazi.

Akitoa taarifa hiyo kwa waandishi wa habari waziri wa ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na serikali za mitaa(TAMISEMI) Mh.SELEMANI JAFO amesema kuwa utenguzi huo umefanyika baada ya kufanyika kwa ziara ya kikazi ya Waziri mkuu wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh.KASSIM MAJALIWA ambapo imebainika wazi kuna watendaji walio chini ya baadhi ya Halmashauri kushindwa kusimamia vyema maeneo yao ya kazi.

Hivyo basi kutokana na hali hiyo ikapelekea Mh.Raisi Dkt.JOHN POMBE MAGUFULI ambaye pia ni mwenye dhamana ya Ofisi ya TAMISEMI kumtengua kiongozi huyo wa halmashauri hiyo Pia waziri JAFO amemwelekeza katibu mkuu  wa wizara hiyo kuwa hamchukulie  hatua stahiki  mweka Hazina aliyehusika wakati wa matumizi hayo mabaya ya fedha za seraikali yaliyofanyika hapo awali.

Aidha amewataka watendaji wote walio chini ya Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kufanya kazi kwa weledi na kuzingatia kanuni za utumishi wa umma na kuahakikisha rasiliamali za Nchi zinatumika kwa maslahi mapana ya Wananchi na Taifa kiujumla.

Post a Comment

 
Top