0











 





 Na.Vedasto George,Morogoro

Kampeini ya moro yetu safi imetekelezwa hileo mala baada ya wananchi na wakazi  wa kata ya mazimbu mkoani Morogoro kujitikeza kwa wingi katika zoezi la kufanya usafi  katika eneo linalo jengwa zahanati ya kata mkoani humo.

Akizungumza mala baada ya kumaliza zoezi la usafi mkuu wa wila ya morogoro mjini Bi. Regina Chonjo   amewashukulu wananchi kwa kujitokeza kwa wingi katika zoezi hilo  na kuwaomba wananchi  kuendelea kutunza mazingira ili kuepuka magonjwa  ya mlipuko yanayo weza kujitokeza ikiwemo kipindu pindu.

   Aidha Bi. Chonjo amewataka wananchi wote mkoani humo  walio na viwanja vikubwa ambavyo  avijaendelezwa kama inavyo takiwa  waviendeleze mala moja  ili kuepuka  usumbufu unaoweza kujitokeza ikiwemo kunyangaywa viwanja hivyo.

 Katika atua nyingine  mkuu wa wilaya ya morogoro Bi. Chonjo amewataka viongozi wa kisiasa mkoani humo kuacha mala moja  kuwapotosha wananchi juu ya  masuala ya maendeleo na kusema kuwa siasa itumike kwa kuleta maendeleo.

Awali akimkalibisha mkuu wa wilaya Mhe. msitaiki meya na diwani kata ya mazimbu Bw. Paschal Kihanga  amebainisha kuwa zoezi la usafi katika kata iyo niendelevu na kuwataka wananchi kuendelea kujitokeza  kwa wingi kila mwisho wa mwezi kufanyausafi ili kuiweka morogoro safi.

Post a Comment

 
Top