0





Image result for baghayo saqware picha


Watumiaji wa bima wanoanunua bidhaa kutoka nje ya nchi wametakiwa kukata bima kupitia makampuni ya ndani ya nchi na sio badala yake kukatama bima kutoka katika makampuni ya nje ya nchi   kwani kuifanya hivyo kutasaidia kuongezeka kwa mapato ya ndani na hata kupelekea     kasi ya kukua kwa uchumi kuongezeka uchumi hapa nchini.

Hayo yamesemwa na kamishina wa bima kutoka mamlaka ya usimamizi wa shuguli za bima Bw.BAGHAYO SAQWARE alipokuwa akifungua semina ya mafunzo kuhusu utumiaji wa mfumo wa kununua bima kupitia matandaoni (TIIP) kwa waandikishaji wa bima kutoka katika makampuni mbalimbali hapa nchini.

Amesema kuwa serikali imekua ikitoa fedha yingi kulipa makampuni ya bima yaliyopo nje ya nchi kwani watumiaji wengi wa bima wanaoagiza bidhaa kutoka nje ya nchi  wamekuwa wakikata bima kutoka katika makampuni ya nje hivyo hali hiyo imekuwa ikichangia kushuka kwa mapato  katika makampuni ya bima hapa nchini na hata kupelekea mapato mengi kutoingia serikali hivyo hali hiyo inaweza kusababisha kasi ya kukua kwa uchumi kupungua.

Pia SAQWARE  ameeleza kuwa ni muhimu  makampuni na watu binafsi wanaotumia bima  kuutumia mfumo wa kukunua bima kupitia matandaoni(TIIP) kwani wasio fanya hivyo watakuwa wanakwenda kinyume na sheria ya bima ya mwaka 2009.

 Hivyo basi  kamishina wa bima anaweza kuwapa adhabu kwa mujibu wa sheria ikiwemo kufutiwa leseni,faini au kosa hilo likijumuishawa katika kuhujumu uchumi itapelekea kujumuishwa katika makosa ya jinai kwaiyo  ni muhimu kuutumia mfumo huo kwani unafaida nyingi kwa watumiji wa bima na Taifa kiujumla.

Aidha nae Raisi wa taasisi ya bima Tanzania(IIT) Bw.BOSCO JAMES amesema kuwa mafunzo hayo kwa waandikishaji wa bima yamelenga kuwaelimisha jinsi ya kutunza taarifa za watumiaji wa bima kupitia matandao hivyo  taasisi hiyo ya IIT  kwa kushirikiana na chama cha wakala wa bima Tanzania(TIBA) pamoja na Mamlaka ya usimazi wa shuguli za bima Tanzania (TIRA) wameshirikiana kuaandaa semina hiyo ili kuwapa uelewa waandikishaji hao. lengo likiwa nikutoa mafunzo yatakayowasidia waandikishija wa bima katika makampuni mbalimbali   kujua jinsi gani ya kuutumia mfumo huo ili  waweze kuelewa jinsi gani  ya kuwaandikisha watu wanaoagiza mzigo kutoka nje ya nchi na kutunza taarifa zao na kufikisha katika mamlaka zinazo husika ili kufanya watumiaji wa bima kukunua bima kutoa ndani ya nchi.

Post a Comment

 
Top