
Na.Martin Joseph
Jamii imetakiwa kujua kuwa utupaji wa taka kiholela hasa taka ngumu pasipo kufuata utaratibu ni moja kati ya vitu vinavyosabisha magonjwa katika jamii,mafuriko na hata kupelekea kuzalisha gesi ambazo zitakuwa na madhara kwa maisha ya viumbe hai hasa hasa binadamu.
Hayo yemesemwa na Kaimu
Mkurugenzi wa baraza la hifadhi na usimamizi wa mazingira (NEMC)
Dkt.VEDAST MAKOTA alipokuwa akifungua mkutano wa siku mbili wa wadau wa kuandaa
mkakati wa kitaifa wa kusimamia taka Tanzania ulioandaliwa na shirika la umoja
wa mataifa la kusimamia mazingira (UN
environment) uliyofanyika Jijini DAR ES SALAAM.
Amesema kuwa kumekuwa na tabia ya kutupa taka
pembezoni mwa barabara kwenye miferejini na hata sehemu
nyingine hivyo hali hiyo imekuwa ikileta madhara makubwa katika jamii na hata kuhatarisha maisha ya viumbe hai mbalimbali hivyo ni vyema jamii ikatumia
utaratibu mzuri katika kutupa taka na hata kutunza mazingira.
Aidha nae mwenyekiti
wa taasisi isiyo kuwa ya kiserikali inayojishulisha na utuzaji wa mazingira hapa
nchini (AGENDA) ambaye pia ni kiongozi wa mradi wa kusimamia taka ngumu
Prof.JAMIDU KATIMA ameiomba serikali kuendelea kushirikiana na wadau pamoja na
taasisi mbalimbali zinazojishulisha na maswala ya mazingira hapa nchini kwani kwakufanya hivyo
kutalinusulu taifa kuondokana na madhara ambayo yanatokana na uchafuzi wa
mazingira.
Post a Comment