
Na.Martin Joseph
Benki kuu ya dunia imehahidi kutoa Dola millioni 300 kwa serikali
ya Tanzania kupitia wizara ya maji na
Umwagiliaji fedha hizo zimetolewa kwa
lengo la kuboresha miradi mbali mbali ya maji
safi na salama maeneo ya vijijini hapa nchini.
Hayo yamesemwa na Naibu
wa waziri wa Wizara ya maji na umwagiliaji JUMAA AWESO alipokuwa akizungumza na
waandishi wa habari Jijini DAR ES SALAAM baaada ya kumaliza kikao kilicho
andaliwa na benki kuu ya dunia kwakushirikaiana na wizara hiyo ambacho walikua wakijadili ni namna gani
wanaweza kuwapatia watu maji safi na salama.
Amesema kwasasa kumekuwa na vituo vichache ambavyo vimekuwa
vikitoa maji kwani vituo vingi vimeshindwa kutoa maji kutokana na sababu za
kiufundi ambapo waandisi wengi wamekuwa wakibuni miradi ya maji kipindi cha
mvua ambapo kipindi hicho uhaba wa maji unakuwa mdogo na watu wengi wamekuwa
wakitumia maji ya mvua hivyo kwa kipindi cha kiangazi miradi mingi huwa
inashindwa kutoa maji kutokana na kukaushwa na jua.
Kwaiyo hali hiyo imekuwa ikiwafanya wananchi wengi hasahasa wa vijijini kuwa na uhaba wa maji hivyo ameeleza kuwa endapo fedha hizo
zitapatikana ataakikisha kuwa anazitumia vizuri kwakukamirisha miradi
mbalimbali ambayo ilikuwa bado ajikamilika na ataakikisha kuwa miradi hiyo
itabuniwa kipindi cha kiangazi na watakao fanya kazi hiyo watakuwa waandisi
kutoka hapa nchini kwani wao kwaasilimia kubwa ndio wanajua shida za maji
zilizopo hapa nchini.
Aidha ametoa wito kwa wananchi kuendelea kutunza mazingira
kwaajili ya kuvisaidia vyanzo vya maji visikauke na hata kupelekea maeneo
mbalimbali kuepukana na uhaba wa maji.
Post a Comment