Imeelezwa kuwa wauguzi na wakunga hapa nchini
wamekuwa wakikumbwa na changamoto mbalimbaliikiwemo kupatwa na matatizo ya
kuumwa mgongo hivyo hali hiyo imekuwa ikiwafanya kushindwa kufanya kazi kwa
muda mrefu kama inavyotakiwa.
Hayo yamesemwa na mkurugezi wa huduma za uuguzi na wakunga
kutoka wizara ya afya,maendeleo ya jamii,jinsi,wazee na watoto GUSTAV MOYO alipokuwa
akitoa taarifa kwa vyombo vya habari katika warsha ya siku moja iliyoandaliwa
na shirika la umoja wa mataifa linalojishulisha na idadi ya watu(UNFPA) kuhusu
kongamano la kisayansi la wauguzi na wakunga linalotarajiwa kufanyika Aprili
Nne na tano mwaka huu mkoani DODOMA huku mgeni rasmi katika kongamano hilo
akitarajiwa kuwa waziri wa wizara hiyo UMMY
MWALIMU.
Amesema kuwa hapa nchini bado kuna uhaba wa wakunga na waguzi hali ambayo imekuwa ikichangia mkunga mmoja
kuhudumia idadi kubwa ya akina mama wajawazito kwa siku bila kupumzika
na muda mwingine mwingine hali hiyo imekua ikiwasabibshia wakunga hao kuiona
kazi hiyo kuwa ngumu hata kuchukua hatua
ya kuacha kzai ya ukunga.
Kwa upande wake katibu mkuu wa chama cha wakunga Tanzania-TAMA,
Dkt. SEBALDA LESHABARI ameeleza kuwa kazi ya ukunga ni moja kati ya kazi ambazo zinahitaji moyo kwani watu wengi
hasa hasa wanawake wamekua wakiimbia
kazi hiyo kutokana na mazingira ya kazi kuwa magumu hali ambayo inachangia
kuongezeka kwa vifo vya akina mama wajawazito na watoto wakati ama kabla ya
kujifungua.
Hivyo ametoa wito kwa serikali na wadau wa afya kutengeza
mazingira mazuri ambayo yanaweza
kuwavutia watu wengine waweze kuingia katika kazi hiyo kwani endapo
wakunga wataongezeka hapa nchini inaweza ikasaidia kupunguza vifo vya mama na mtoto.
Pia ameeleza kuwa ni
vyema wananchi wakatambua kuwa taaluma ya ya ukunga ni moja kati ya taaluma
ambazo zinatakiwa kuheshimika kwani watu wanaotakiwa kuingia katika taaluma
hiyo ni wale wenye ufaulu mzuri na sio badala yake kuwa na watu wasio na ufaulu
mzuri kwa watukua wanatoa huduma ambazo hazitakuwa bora kwa wagonjwa.
Post a Comment