Waziri
wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mahmoud Thabit Kombo
amewasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya wizara yake kwa mwaka wa fedha
2025 / 2026, jijini DODOMA
leo Mei 28,
2025.
Waziri
KOMBO
ameliomba bunge lipitishe bajeti hiyo ambayo ni kiasi cha shilingi Bilioni 340.5
ikiwa na vipaumbele vitano.
Aidha
amewataka wabunge kutumia fursa ya kuzungumza na mabalozi waliofika nchini kwa
ajili ya mkutano wa diplomasia ili kuwasaidia kupata wawekezaji katika
miradi mbalimbali ndani ya majimbo yao.
Kadhalika
waziri KOMBO
amezitaka sekta binafsi
nchini kushiriki kuchangia fursa zitokanazo
na diplomasia kiuchumi kupia uwili yaani kikanda na kimataifa kwani ufanya
hivyo itasaidia kutoa ajira kwa vijana wengi wa Kitanzania.
Amehitimisha
kuwa Jumla ya wataalam kumi na saba kutoka nchini QATAR
wamekuja
TANZANIA
kwa ajili ya kutoa mafunzo kwa madereva ambapo katika mafunzo hayo watapata
kupewa ujuzi wa kufahamu magari yanayoendeshwa kidijitali.
Post a Comment