0

 


Serikali imeingia makubaliano na nchi mbalimbali ili kurahisisha utaratibu wa viza ambapo raia wa nchi 71 hawahitaji viza wanapoingia nchini.

Hayo yamesemwa  na Naibu Waziri wa maliasili na utalii  DUNSTAN KITANDULA, alipokuwa akijibu swali la Mbunge  Dkt. Pius STEPHEN CHAYA,aliyetaka kujua ni jitihada gani zimefanyika kurahisisha upatikanaji wa VISA kwa Watalii wenye uraia tofauti wanaokuja nchini.

 Amesema  Serikali imeendelea kuboresha utaratibu wa utoaji wa viza nchini ili kuendana na mabadiliko ya teknolojia duniani ambapo kupitia  Idara ya Uhamiaji imeanzisha mfumo wa maombi ya viza kwa njia ya mtandao (e-Visa) unaowawezesha watalii kuomba viza popote walipo duniani.
ameongeza kuwa Serikali imeboresha Kanuni za Uhamiaji za mwaka
2023 (GN 428) ambapo kwa sasa watalii wanaotumia Visitors Pass wanaruhusiwa kutembelea Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki na kurejea TANZANIA bila hitaji la kuomba upya pasi ya kuingia nchini.

 

 

 

 

Post a Comment

 
Top