0




 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj4zQiSeRrJQhWxe93Iy-102cGsjKStnwxaCq6iZnZy07VKJp5x116vBX_k0r9SydTt3LHtSDPP7OUNb_WQaeTL1y-xCg3xbLMB3apE9X2DmHFVLWy_knMzcK3oXlPX5fF_vobU1cbGxZqt/s640/JKCI.PNG

 Wananchi wametakiwa kupewa elimu juu ya kujikinga na ajali za barabarani kwani kufanya hivyo itasaidia kupunguza idadi ya ajali za barabarani na hata kupunguza kwa kiasi kubwa  ongezeko la wagonjwa wanavunjika viungo Mahospitalini.

Hayo yamesemwa na Dkt.bingwa wa mifupa na mishipa  amabaye pia ni  kaimu mkurugenzi wa kitengo cha Moi muhimbili Dkt.SAMWELI SWAI alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu njia zinazotumika katika kuwatibu watoto wenye matatizo ya vichwa,migongo wazi na waliopata ajali na kuvunjika viungo.

Amesema  kumekuwa na ongezeko kubwa  la wagonjwa  katika kitengo hicho walivunjika viungo  kutokana na ajali za barabarani  hasa hasa waendesha pikipiki maarufu kama boda boda kwani wamekuwa wakizadharau sheria za barabarani na elimu  zinazotolewa na vyombo mbalimbali vya usalama ikiwemo kitengo cha usalama barabarani pamoja na vyombo vya habari.

Hivyo basi Dkt.SAMWELI ameeleza kuwa kitengo hicho cha Moi  kwakushirikiana na vyombo mbalimbali vya usalama barabarani waatakikisha kuwa wanaendelea kutoa elimu kwa wananchi ili kupunguza kabisa tatizo la  ajali za barabarani.
 Wakati huo huo taasisi ya moyo ya jakaya kikwete(JKCI)kwa kushirikaiana na taasisi ya Okoa Moyo wa mtoto(SACH) wameweka  kambi  ya siku tano katika Hospitali ya  taifa ya muhimbili kwa lengo la kufanya upasuaji wa bila kufungua kifua kwa watoto,uchunguzi wa moyo kwa watoto,utohaji elimu ya upasuaji wa moyo bila kungua kifua na jinsi ya kuwa hudumia watoto waliofanyiawa upasuaji huo.

Taarifa kutoka katika taasisi hiyo  zinaeleza kuwa mbaka sasa watoto 15 wenye matatizo ya moyo wameshafanyiwa upasuaji na watoto 32 wamefanyiwa uchunguzi wa moyo ambapo watoto 20 wamefanyiwa matibabu katika kambi hiyo na wenngine 12 waliobaki watatibiwa na madakatri wa ndani kuanzia wiki ijayo.

Post a Comment

 
Top