
Mahakama ya Tanzania
pamoja na wadau muhimu katika sekta ya Sheria wamewataka wananchi kuhudhuria maadhimisho ya
wiki ya sheria nchini kwa lengo la
kufikia Dira ya Upatikanaji wa haki kwa
wakati.
Akizungumza Na Waandishi wa habari leo jijini
Dar es salaam Jaji Mkuu wa Tanzania Prof
Ibrahim Hamis Juma ameeleza kuwa kwa mujibu
wa Ibara ya 107A ya katiba imepewa Mamlaka ya mwisho katika utoaji
haki,hivyo huadhimisha siku ya Sheria
itakuwa tarehe 1 februari mwaka huu ni siku maalum ambayo itaashiria kuanza
rasmi kwa shughuli za mahakama kwa mwaka huu.
Jaji Mkuu Ibrahim ameweza kubainisha kuwa Mahakama ya
Tanzania pamoja na wadau muhimu katika Sekta ya sheria
watatumia siku tano kuanzia tarehe 27
hadi 31 Januari mwaka huu kutoa elimu yaSheria kwa wananchi watakaopata nafasi
ya kuhudhuria.
Wakati akizungumzia
swala hili ameitaka jamii kuzifahamu
shughuli mbalimbali zinazofanywa na Mahakama pamoja na wadau wa Sekta ya
Sheria ili kufikia Dira ya upatikanaji
wa haki kwa wakati.
Aidha,Jaji Mkuu Ibrahim ametoa wito na kusisitiza kuwa Wananchi na wadau
wote wa Sheria wanaombwa kutembelea
katika Viwanja vya Mnazi Mmoja kwaajili ya kujifunza na kupata huduma
mbalimbali za kisheria kutoka kwa majaji,mahakimu,wasajili watendaji,Mawakili
wa serikali na Mawakili wanaojitegemea ambao watakuwa tayari kuwasikiliza na
kuwahudumia ipasavyo.
Post a Comment