
Serikali ya Tanzania
kupitia wizara ya Afya,Maendeleo ya jamii,Jinsia,Wazee na Watoto leo imeungana
na mataifa mengine ulimenguni kote katika
kuhadhimisha siku ya ukoma
Duniani siku hiyo inafanyika kila jumapili ya mwisho wa mwezi januari
ulimwenguni kote.
Akizungumza na waandishi wa habari naibu waziri wa Wizara ya
Afya,Maendeleo ya jamii,Jinsia,Wazee na
Watoto Dkt.FAUSTINE NDUGULILE kwa niaba
ya waziri wa wizara hiyo amesema kuwa kwa mwaka huu siku hiyo imehazimishawa
leo katika makao makuu ya wizara hiyo Jijini DAR ES SALAAM.
Pia maadhimisho hayo yanatumika kama
njia ya kuelimisha na kuongeza uelewa duniani kuhusu ugonjwa huo wa kale ambao unatibika
na mgonjwa kupona kabisa vile vile Dkt.NDUGULILE ameeleza kwamba nchi yetu
ilifikia viwango vya kitaifa katika kutokomeza ukoma mnamo mwaka 2006 kwa
kiwango cha chini ya mgonjwa mmoja kati ya watu 10,000 lakini ungonjwa huo bado
umeendelea kuwa tatizo la kiafya miongoni mwa jamii mbalimbali hapa nchini.
Hivyo basi serikali kwa kulitambua hilo inatumia njia
mbalimbali katika kudhibiti ugonjwa huo hapa nchini ikiwemo kuendesha kampeni
za uibuaji wa wagonjwa wapya ngazi ya jamii kwa kushirikiana na watoa huduma
katika ngazi hizo pia utekelezaji wa mpango wa majaribio ya utohaji wa dawa
kinga katika ngazi ya kaya kwaajili ya kuzui maambukizi ya ungonjwa huo.
Aidha naibu waziri huyo ametoa wito kwa wazazi na walezi kujijengea
tabia ya kuchunguza miili yao na ya watoto wao ili kungundua kama wanadalili za
ungonjwa huo na endapo mzazi au mlezi
atagundua kuwa yeye au mtoto anadalili za ukoma hivyo anatakiwa kuwai au
kumuwaisha muathirika wa ungonjwa huo
mapema katika vituo vya afya ili kupatiwa matibabu kwani ugonjwa huo
unatibika bure na dawa zinatolewa bure katika vituo vyote vya Afya hapa nchini.
Post a Comment