0











 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgvvozE80hstWXk0pYTwuXAlclMvxMiiB1JNTS6yOS8-76F03XZk3P3sVj717wzt3qA7aUUb84Uco3yXtZ6640SxlK5NhP1yE9uV2hp2v5jZqPYs4brUipU21H2RXiQDdhqFweSL9g_8e4f/s1600/MASS1-768x510.jpg









Baraza la taifa la usalama barabarani limewataka wamiliki wa magari binafsi kupelekeka magari yao katika vituo vya polisi na maeneo yaliyotegwa kwa ajili ya ukaguzi pindi ifikapo tarehe moja march mwaka huu kwani kufanya hivyo itasaidia kupunguza ajali za barabarani hapa nchini.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi na mwenyekiti wa baraza hilo mhandisi HAMAD MASAUNI alipokuwa akitoa taarifa ya tathimini ya utendaji na utekelezaji wa awamu ya pili ya mpango mkakati wa baraza la taifa la usalama barabarani wa kupunguza ajali za barabarani kwa asilimia 10 katika kipindi cha miezi sita kuanzia julai hadi desemba 2017.

Amesema kuwa tamko hilo limetoka ikiwa ni baada ya baraza hilo kujilizishwa na mafanikio yaliyopatikana  na utekelezaji wa   mpango mkakati wa awamu ya pili wa  kupambana  na ajali za barabarani kwakufanya ukaguzi wa magari ya biasahara,abiri na yakubebea mizigo hivyo ni vyema wamiliki wa magari binafsi wakalitii agizo hilo pasipo shuruti.

Aidha Ametoa wito kwa kampuni zinazouza pikipiki hapa nchini kuacha kuuza pikipiki zilizosajiliwa kwa majina ya kampuni zao kwani kitendo hicho ni  kinyume cha  sheri  na kimekuwa kikisababisha usumbufu mkubwa wakati wa ukamataji wa pikipiki zinazokamatwa kwa uvunjifu wa sheria za barabarani  na makosa mbalimbali.

Post a Comment

 
Top