0







 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhGMuLBtK8_VQ33rE-gyhGU5UBCbJ-mdc0RoNo1b47HkDAie5QuEUu4t0goPnQugTWgDgHawqLUCXrE-8nnVApj4oheCaCeUGrUW5g9em9iT8-TSmNuHtVTPwn99JFqyI0UXtOUhOzXLko/s1600/03.JPG










Wananchi pamoja na sekta mbalimbali hapa nchini wametakiwa kutambua kuwa teknolojia ya habari na mawasiliano(TEHAMA)ni moja kati ya vitu vinavyo changia katika ukuaji wa maendeleo hapa nchini hivyo ni vyema wakaitumia vizuri ili iwasidie katika  kujiingizia  kipato na hata kuwaondoa katika umaskini.

Hayo yamesemwa na Mkurugezi wa tume ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano(TEHAMA) SAMSON MWELA alipokuwa akifungua mkutano wa jukwaa la tahama salama Tanzania (CYBERTZ) uliyofanyika Jijini DAR ES SALAA.

Amesema kuongezeka kwa matumizi ya  tehama hapa nchini imeleta mchango mkubwa katika maendeleo ya jamii na kiuchumi kwani imesaidi kuwaunganisha wananchi katika maeneo mbalimbali na huduma za kifedha na mabenki  hivyo ni vyema wakatambua kuwa tehama ni  sehemu muhimu  katika maisha yetu ya kila siku na usalama wake ni muhimu kwa ustawi. 

Pia ameeleza changamoto mbalimbali zinazosababishwa na matumizi yasiyo rasmi ya Tehama hapa nchini ikiwa ni pamoja na maudhi yasiyo endana na maadili ya kitanzania,watu kutumia mitandao kuchafuana,wizi na hujuma kwa njia ya mitandao na udukuaji wa taarifa kinyume na taratibu.

Aidha ametoa wito kwa wadau wa jukwaa la tehama salama Tanzania walioshiriki katika mkutano huo kuendelea kuwa na ushirikiano na kubadilishana uzoefu walio nao ili kulifanya jukwaa hilo lizidi kusonga mbele na kuendelea kutetea masilahi ya Teknolojia ya habari na mawasiliano hapa nchini.

Post a Comment

 
Top