0



 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhppza34csTqNYR8oaNzEi2nQw30rTs6owCBwJJ-dSanDTJBlZivuT2aUv3Gz4u5Mp8q576woYeZ8Zd2IBTZNEzfAyAQH2YJH1VjgVSxYwwV5DroTqxYYuKLxdtlOgd_LpRX7m4ZGiFMV_L/s1600/DSC_5129.JPG















Serikali ya Tanzania kupitia wizara ya maliasili na utalii imekutana na serikali ya china ili kujadili jinsi ya kukuza maendeleo katika sekta ya utalii baina ya nchi hizo mbili.
Akizungumza na waandishi wa habari Jijini DAR ES SALAAM  katibu mkuu wa wizara ya  maliasili na utalii meja jenerali GAUDENCE MILANZI amesema  kuwa   Tanzania na China  zinashirikiana katika mambo mbalimbali ambayo yanapelekea nchi zote mbili kupata maendeleo kupitia ushirikianao huo.
Hivyo basi katika kuendelea kuimalisha ushirikino huo serikali ya  Tanzania kupitia wizara ya maliasili na utalii ikaamua kukutana na nchi ya China  ili kujadili njia zitakazo ifanya sekta ya utalii iweze kutangazika  kitaifa na hata kimataifa kwa lengo la kuifanya sekta hiyo ikue  kimaendeleo hapa nchini na hata kupelekea ukuaji wa uchumi uzidi  kuongezeka.
Pia Jenerali MILANZI ameeleza kuwa majadiliano hayo yamelenga   kulikumbusha Taifa  la  china kuwahamasisha wananchi wake  kuja wingi hapa nchini kwajili ya kufanya  utalii kwani kumekuwa na watalii wachache wanao toka katika taifa hilo hivyo kupitia majadiliano hayo yatapelekea   kupata watalii wengi kutoka nchini humo.
Aidha nae balozi wa china hapa nchini Bi.WANG KE amesema kuwa nchi ya China itaendelea kuisaidia kwa nguvu  serikali  ya Tanzania katika kuhakikisha sekta ya utalii inakuwa  kimaendeleo  na pia wataakikisha kuwa wanapiga vita ujangili  nakutoa elimu  kwa jamii ya china iliyopo nchini Tanzania juu ya kuwalinda wanayapori dhidi ya ujangili.

Post a Comment

 
Top