0


 
https://tse3.mm.bing.net/th?id=OIP.P4JnuCsV63AENVji1O2tAgHaDu&pid=15.1&P=0&w=355&h=180Watanzania wametakiwa kuitunza na kuindeleza histori ya afrika kwani itasaidia kukilithisha kizazi kijacho historia nzuri na itakayowajenga zaidi na hata kuwanufaisha zaidi katika maisha yao ya hapo baadae.
 Hayo yamesemwa na Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Dkt. HARRISON MWAKYEMBE alipokuwa katika mkutano na waandishi wa habari Jijini DAR ES SALAAM akitoa ufafanuzi kuhusu ujenzi  wa kituo kikuu cha kumbukumbu ya ukombozi wa bara la Afrika kinachotalajiwa kujengwa katika eneo la MWABEPANDE  Jijini DAR ES SALAAM.
Amsema histori ya Afrika inawategemea Waafrika wenyewe hivyo ni vyema Watanzania wakatambua kuwa ni muhimu kuisimamia vyema historia hiyo ili isaidie kwavizazi vinavyokuja na wajue kuwa  walipotoka ni wapi  na wanapokwenda ni wapi kwani hii itakua faida kubwa katika maisha yao.
Pia kwa upande mwingine waziri MWAKYEMBE ameushukulu ubalozi wa URUSI pamoja na shirika la maendeleo la umoja wa mataifa(UNDP) kwakukubali  kushirikiana na serikali katika kufanikisha mradi huo ambao utasaidia katika kutunza historia mbalimbali za Afrika pamoja na zile za  Tanzania.
Aidha ametoa wito kwa wananchi hasa hasa vijana kuvitumia vivutio vilivypo hapa nchini ambavyo vimetumza historia mbalimbali  kama fursa ya kujipatia kipato kwa watu watakao jitokeza kutembelea maeneo hayo kwa lengo la kufanya utalii.

Post a Comment

 
Top