0





 https://swahilitimes.com/wp-content/uploads/2017/05/xMatataG_4336-6-702x375.jpg.pagespeed.ic.DhGk6kVhjV.jpg



Serikali kupitia ofisi ya taifa ya Takwimu imetoa takwimu ya  mfuko wa bei za bidhaa katika Taifa kwa mwezi Desemba mwaka jana pamoja na mwezi Januari mwaka huu ambapo imeelezwa kuwa  kasi hiyo imebaki kuwa sawa ambapo  mwezi januari mwaka huu  emebaki kuwa asilimia 4 ambapo ukilinganisha na hile ya   mwezi desemba mwaka jana.

 Hayo yamesemwa na  mkurugenzi wa sensa na takwimu za jamii kutoka katika ofisi za Taifa ya Takwimu(NBS)EPHIAM KWESIGABO alipokuwa akitoa taarifa kwa vyombo vya habari  Jijini DAR ES SALAAM kuhusu kasi ya mfumuko wa bei za bidhaa na huduma zinazotumiwa na kaya binafsi nchini.

Amesema kuwa hali hiyo imebaki kuwa hivyo kutokana na kazi kubwa inayofanywa na serikali ya kuhakikisha  kuwa  miradi mbalimbli ambayo ilikuwa ikichangia mfumuko wa bei za bidhaa na huduma nyingine kuongezeka hivyo nivyema wananchi wakaendelea kuiunga mkono  serikali katika kuhakikisha bei za bidhaa hapa nchini inakuwa nzuri.

Aidha KWESIGABO ameeleza baadhi ya bidhaa za vyakula zilizochangia mfumuko wa bei kufikia asilimia 4 kwa mwezi januari mwaka jana na mwezi januari mwaka huu ambapo mahindi kwa asilimia 8,Maharage kwa asilimia 4.3,Samaki kwa asilimia 9 na ndizi za kupikia kwa asilimia 9.





Post a Comment

 
Top