Wakulima nchini wametakiwa kushiriki katika semina na mikutano mbalimbali inayo husika na maswala ya kilimo kwani kufanya hivyo itawasaidia kupata fursa na ufahamu wa kujua njia za kujikwamua kupitia kilimo.
Hayo yamesemwa na
mkurugenzi wa mtandao wa kijani kibichi Tanzania (MKIKITA) ADAM NGAMANGE alipokuwa
akitoa taarifa kwa vyombo vya habari Jijini DAR ES SALAAM kuhusu mkutano wa
kutoa mafunzo kwa wakulima ulioandaliwa na Mtandao huo kwakushirikiana na
taasisi inayojishugulisha na utoaji wa mafunzo kwa wakulima(ALL FOR ALL
FOUNDATION) unaotalajiwa kufanyika Februari 24 mwaka huu Jijini DAR ES SALAAM.
Amesema kumekuwa na wakulima wachache wenye uelewa kuhusu
kilimo bora na chenye manufaa hivyo hali imekua ikipelekea uzalishaji wa mazao
kuwa mdogo na hata kuwafanya wakulima
wengi kuwa maskini kutokana na kukosa
njia ambazo zingewasaidia kuondokana na tatizo hilo ambalo limekuwa
likiwakabili wakulima wengi hapa nchini.
Hivyo basi Mtandao wa
kijani kibichi kwa ushirikiana na taasisi inayojishugulisha na kutoa mafunzo
kwa wakulima wakaamua kuanzisha mafunzo hayo kwa lengo la kuwasaidia wakulima
kujifunza mambo mengi ya kilimo ili kuboresha kilimo kwa kila mkulima aliyekuwa
hapa nchini ili iwasaidie katika kupata maendeleo yao binafsi na hata ya taifa kwa
ujumla.
Aidha NGAMANGE ameiomba serikali iendelee kushirikiana na
watu binafsi pamoja na mitando mbalimbali inayojishugulisha na maswala ya
kilimo ili kuwasaidia wakulima kulima
kilimo bora na kupata masoko mazuri ambayo yatawafanya wakulima kuuza bidhaa
zao kwa uraisi na kupata kipato kitakacho wasaidi na hata kuondokana na wimbi
la umaskini.
Post a Comment