0
















 Image result for mkurugenzi wa jiji la dar

Na.Martin Joseph
Meya wa   Jiji la DAR ES SALAAM ISAYA MWITA  amemtaka mkurugenzi wa jiji hilo Bi.SPORAH LYANA  pamoja na  kamati yake kusimamia na kurekebisha bajeti  pamoja na makusanyo mbalimbali kwani kwakufanya hivyo kutasaidia kutekeleza miradi mbalimbali ya kimaendeleo ndani ya jiji hilo.

Meya huyo ameyasema hayo Jijini DAR ES SALAAM  wakati akizungumza na waandishi wa habari baada ya kumaliza kikao cha kupitia taarifa mbalimbali zilizo wasailishwa na wanakamati waliochanguliwa na baraza hilo. 

Amesema kuwa  ukusanyaji mapato na mambo mengine katika Jiji hilo yanakwenda Vizuri kwani  mwaka wa fedha wa serikali uliyoisha mwezi oktoba  mwaka jana walikusanya asilimia 54 ya bajeti yote zilizopangwa na serikali kwaiyo wanatalajia mbaka ikifika mwaka mpya wa serikali unaoanza mwezi july mwaka huu wanaweza wakaweka rekodi katika upande wa ukusanyaji mapato na bajeti yote kwa ujumla hivyo ameeleza kuwa katika kuyatimiza hayo nivyema ukusanyaji wa mapato ukasimamiwa vyema ili malengo hayo yeweze kutimia. 

Pia ameeleza kuwa  katika juhudi za kufanya   ukusanyaji mapato unaongezeka katika jiji hilo wamehamua kuziwekea kipaumbele shuguli za utalii kwani kwasasa wanavisiwa ambavyo vinatumika kwa shuguli hizo na pia wanatajia kuongeza wanyama ambao watatumika katika kuwavutia watu kufanya utalii kwa asilimia kubwa jijini hapo na kufanya mapato yazidi kuongezeka.

Aidha amezitaka halmashauri zote za Jiji la DAR ES SALAAM kuwasajili watu watakao tumika kwajili ya kuzika   watu wasio kuwa na ndugu kwani kwasasa sheria inawaruhusu  kufanya hivyo kwa mtu yoyote yule ambaye amekumbwa  na matatizo hayo.

Post a Comment

 
Top