0

  Image result for FATMA MJUNGU
Wananchi wameombwa kujitokeza kwa wingi katika vituo vya kuchangia damu ili waweze  kuchangia damu hasa kipindi hiki cha chakuelekea sikuu ya pasaka kwani bado kumekuwa na wahitaji wengi wa damu katika hospitali  mbalimbali hapa nchini.

Hayo yameelezwa  na Afisa Mhamasishaji kutoka wizara Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Bi.FATMA MJUNGU   wakati akizungumza na waandishi wa habari katika zoezi la uchangiaji wa damu lililikua likifanyika  eneo la Kariakoo Jijini DAR ES SALAAM.

Amesema kumekuwa na changamoto kubwa kutokana na kutokuwa na muitikoa wa watu wengi kujitokeza kuchangia damu hususani kwa wanawake hivyo hali hiyo imekua ikipelekea kuwepo kwa uchache wa damu katika vitu vya afya mbalimbali na hii imekua ikisababisha watu kushindwa kupata damu kwa wakati pale wanapohitaji.


Pia  ameeleza kuwa mahitaji ya damu kwasasa yamekuwa  ni mengi hasa  kwa  watu wanaofanyiwa upasuji hivyo upungufu  wa damu katika vituo vya afya unaweza ukapelekea watu hao kupoteza maisha kwasababu zisizo kuwa za msingi.

Aidha kwa upande mwingine  nae mmoja katika ya watu waliojitokeza kuchangia damu katika eneo hilo HASSAN SAID amesema kuwa swala la kuchangia damu ni sehemu ya kutoa sadaka kama unavyo toa sadaka nyingine kwa kuokoa maisha ya watu hivyo nivyema wananchi wakatambua kuwa ni muhimu kuchangia damu ili kuokoa  maisha ya watu.

Post a Comment

 
Top