Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) leo imezindua Rasmi mfumo
wa utoaji vitambulisho kwa wafanyabiashara wadogo ambao wapo kwenye sekta hiyo
wakiwemo wamachinga.
Akizungumza katika uzinduzi huo uliyofanyika Jijini DAR ES
SALAAM Kamishina wa mamlaka hiyo CHARLES KICHERE amesema kuwa utohaji wa
vitambulisho kwa wafanyabiashara hao unatokana na marekebisho ya sheria ya
usimamizi wa kodi ya mwaka 2015 yaliyofanyawa na kikao cha bunge la bajeti la
mwaka wa fedha 2017/18 ambapo moja ya marekebisho hayo ni kuwatambua na
kuwapatia vitambulisho maalum wafanyabishara wadogo.
Pia ameeleza kuwa zoezi hilo linatekelezwa na mamlaka ya
mapato Tanzania kwa kushirikiana na mamlaka ya Vitambulisho vya
Taifa(NIDA),Tawala za Mikoa na serikali za Mitaa(TAMISEMI),Wakala wa
usajili,Ufilisi wa Udhamini(RITA) pamoja na Idara ya uhamiaji.
Aidha ametaja njia ambazo wafanyabishara wadogo wanahitajika
kuzitumia pindi wanapohitaji vitambulisho hivyo maalum ikiwemo kujiunga katika
vikundi maalum vinavyotambuliwa kisheria na serikali,kuwa na kitambulisho cha
Taifa,kuwa na namba ya Utambulisho wa Mlipakodi ya vikundi wanavyojiunga pamoja
na kuchangia shilingi elfu 10,000.
Post a Comment