
Tafadhari rejea mkutano wa waandishi wa habari
uliofanyika mnamo tarehe 8/03/2018 katika ukumbi wa Mwl J.K Nyerere,
uliohitishwa na Mweshimiwa Dr. Harrison G . Mwakyembe.
Kwanza
kabisa pokeeni Shukrani kutoka kwa Kamati kuu ya Taasisi Hii ya
kimataifa ya Wataalamu wa Lojistiki na Usafirishaji kwa mwitikio wenu.
Tayali
Raisi wa Taasisi na Katibu Mkuu wamesafiri Kwenda Nigeria kuhudhuria
mkutano hou wa Afrika pamoja na wajumbe wengine wanne, wanatarajiwa
kurudi Nchini mnamo tarehe 17 mwezi huu.
Tafadhali
rejea kichwa cha habari, Moja ya yaliyozungumzwa siku tajwa ilikua ni
pamoja na mimi mtanzania mwenzenu kukabidhiwa Cheti kama zawadi ya Kua
Miongoni mwa Washindi sita Duniani wa tuzo ya mtaalamu bora kijana
kimataifa katika usafirishaji na Lojistiki pamoja na washindi wengine
watano ambao ni Sonia Man-yee kutoka China, Muhammad Refayet Choudhury
kutoka Bangradesh, Jenna Hood kutoka Australia, Jesaya Mwadingi kutoka
Namibia, na Virginia Christians kutoka Newzeland.
Kwa
kusema hayo ningependa kuambatanisha Taarifa yangu Fupi inayohusu
Historia yangu na jinsi nilivyofika hapa nilipo. Ninaomba Iandikwe
kwenye magazeti iwe kama Chachu ya kuonesha mwanga kwa vijana wengine
wenye taaluma mbalimbali, pia nipo tayari kufanya mahojiano na katika
vipindi mbarimbari vya radio na runinga, bila kusahau mitandao mingine
yote ya kijamii kwa manufaa ya Taifa kwa ujumla.
Post a Comment