0





 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjmdkofYGTxTfQ9brzw3P7xA8Hj8DFnlS-DV2T1UOxU7B4xtV7q0c7T56I0iQ0PtvuO2thtShhcE1QugNLDIyqjGIA6OldSL-KNHMs4wcLkz64NyDYtk-9Qh_3OckHxO8_JBJ7RoSp4m4k/s1600/1.jpg 

Serikali kupitia Wizara ya Kilimo imesema inaendelea kushirikiana na mashirika ya kigeni ambayo yanawekeza katika masuala ya kilimo ili kumsaidia mkulima kujikwamua kiuchumi kupitia vyama vya ushirika.
Hayo yamesemwa leo jijini Dar es salaam  na Mkurugenzi Idara ya Usalama wa Chakula kutoka Wizara hiyo Elimpaa Kiranga wakati wa mahojiano na wahabari mara baada ya uzinduzi wa wa program ya miaka mitano ambayo imeandaliwa na shirika la Weeffect  kutoka nchini Sweeden ambalo limekuwa likifanya kazi na vyama vya ushirika hapa nchini.
Amesema kuwa serikali ya awamu ya tano inahakikisha  hatua hiyo inawanufaisha wakulima wa jinsia zote ambao wamejiunga katika vikundi kwa ajili ya kufanya shuighuli za kilimo ili kusaidia kuboresha maisha yao na Taifa kwa ujumla.
Awali akizungumzia mradi huo Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Weeffect George Onyango amesenma program ya miaka mitano inatarajiwa kutumia kasi cha shilingi za kitanzania bilioni 120 kwa ajili ya kufanya kazi na vyama vya ushirika vipatavyo 11 nchini Tanzanaia,huku akiomba serikali kuweka mbinu na sheria za kilimo zitakazowezesha mkulima  kutoka katika umasikini.

Naye Mtendaji Mkuu wa Benki ya Uchumi Angela Moshi amesema kwamba hadi sasa benki hiyo imewakopesha wananchi kiasi cha shilingi bilioni 19 huku asilimia 30 ya fedha hiyo ikienda kwa wakulima ambapo wamekuwa wakiongeza uzalishaji.
INSERT.3.ANGELA MOSHI.

Post a Comment

 
Top