Na.Martin Joseph
Wananchi wameombwa kupima kupima afya zao ili kuepukana na
magonjwa mbalimbali ikiwemo ugonjwa wa shindikizo la macho kwani ugonjwa huo
umekuwa ukisababisha athari kubwa nakupelekea watu kupata upofu wasioutalajia.
Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya
jamii,Jinsi,Wazee na Watoto Dkt.FAUSTINE NDUGULILE alipokuwa akitoa tamko
kuhusu maadhimisho ya wiki ya kuongeza uelewa kuhusu ugonjwa wa shindikizo la
macho yenye kaulimbiu isemayo “okoa uoni wa macho yako’’iliyoanza hapo jana na
inatalajiwa kuhitimishwa Machi 7 mwaka huu duniani kote.
Amesema kuwa ugonjwa huo ni moja kati ya magonjwa ya macho
yanayoshambulia mshipa wa fahamu wa binadamu unaopeleka mawasiliano ya uoni
kwenye ubongo ili kuweza kutafsiri kile unachokiona hivyo unaweza ukamsababishia
mtu kupata upofu wa taratibu na hatimaye kushindwa kuhona kabisa.
Pia ameeleza kuwa ugonjwa huo unachangia kwa asilimia 15 ya
watu wasiiona na unawaathiri Zaidi watu wenye umri kuanzia miaka 40 na Zaidi kwani wengi wao wamekuwa
hawana tabia ya kuchunguza Afya za macho
kama inavyo shauriwa na wataalamu hivyo basi ni muhimu wananchi wakapima afya
za macho angalau mara moja hasa hasa kwa makundi yaliyo hatarini kupatwa na
ugonjwa huo.
Aidha kwa upande mwingine NDUGULILE amseema maadhimisho hayo
yatakuwa niyakutoa elimu na upimaji wa Afya ya macho kwenye klinki za macho
kwaiyo ametoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kwenye kilnki na vituo vyote vya afya vilivypo hapa nchini kwa lengo la kupimwa na kuchungunzwa kama watakua na dalili
zinazo sababisha ugonjwa huo ili waweze kupatiwa matibu haraka ilikuepukana na
ugonjwa huo ambao ni tishio hapa nchini na duniani kote.
Post a Comment