0




                                                                              
                                                                            
                                                                            


Waajili nchini wametakiwa kulejesha kwa wakati makato ya wafanyakazi  wao  kwenye bodi ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu kwani kufanya hivyo itawasaidia wanafunzi waliokua  vyuoni kuendelea kupata mikopo kwa wakati na hata kuanza masomo yao kwa wakati maalumu pasipo usumbufu wowote.

Hayo yamesemwa na mkurugenzi msaidizi urejeshaji mikopo kutoka katika bodi ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu(HESLB)Bw.FIDERISI JOSEPH alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari wakati akiwa katika  kampeni ya kutembelea makampuni na taasisi mbalimbali ambazo bado hazija rejesha  madeni ya makato  wanayo daiwa na  bodi hiyo.
Amesema kuwa waajili wengi wamekuwa wakiyadhalau makato  hayo na hata kushindwa kuyawasilisha kwa wakati katika bodi hiyo hivyo hali hiyo husababisha  madeni hayo kuongezeka katika makampuni mbalimbali  na kupelekea serikali kushindwa kua na fedha za  kutoa mikopo kwa wanafunzi wanaoingia vyuoni pindi wahitajipo mikopo hiyo.

Pia FIDERISI ametoa ufafanuzi juu ya  kampeni inayofanywa na bodi hiyo ya kutembelea makampuni na taasisi  niya miezi mitatu na kwa sasa inafanyanyika Jijini DAR ES SALAAM kwa mwezi moja  na  mienzi itakayo bakia itaanza kuzunguka katika mikoa minginea hapa nchini lengo nikuwakumbusha na kutoa elimu  waajili kulipa makato kwa wakati na muda walipangiwa. 

Aidha ametoa wito kwa makampuni na taasisi zote hapa nchini ambazo hazijawasilisha makato  wanayo daiwa na bodi hiyo kuyarejesha mapema  makato hayo kwani yapo  kisheria na asiye fanya hivyo atachukuliwa hatua za kisheria na hata kulipishwa faini au kifungo cha miaka mitatu.


Post a Comment

 
Top