0
Shirikisho la vyama vya mogonjwa yasiyo ya kuambukiza Tanzania(TANCDA) limetakiwa kuongeza juhudi za  kutoa elimu kwa wananchi juu ya magonjwa yasiyo ya kuambukiza kwani kufanya hivyo kutawezesha familia nyingi kutopata magonjwa hayo na hata kwa wale ambao wameathirika kuwa na elimu sahihi ya kuyadhibiti magonjwa hayo.

Hayo yamesemwa na kaimu mkurugenzi wa magonjwa yasiyo yakuambukiza kutoka Wizara ya Afya Dkt.SARA MAONGEZI alipokuwa akipokea tunzo ya kimataifa  ya hamasa kwa jamii juu ya ufahamu wa magonjwa yasiyo yakuambukiza ambayo imetolewa na shirikisho la kimataifa la magonjwa yasiyo yakuambukiza (Global NCDs Alliance) wakishirikiana na Falme za kiarabu za mji wa Sharja.

Amesema kuwa magonjwa hayo yamechangia kuongezeka kwa idadi kubwa ya vifo hapa nchini na hata kuwa ni moja ya sababu za tishio la uhai wa binadamu duniani kwa sasa kwani asilimia 27 ya wananchi wanaofaliki huwa wanakufa kwa magonjwa hayo  hivyo ni muhimu shirikisho hilo kutoa elimu hiyo ili kuliepusha taifa kutumia fedha nyingi katika kutibu magonjwa hayo na hata kuepusha watu wengi kufa mapema.

Pia Dkt SARA ametoa wito kwa wananchi kuzingatia elimu wanayopewa kupitia taasisi mbalimbali na vyombo vya habari juu ya magonjwa yasiyo ya kuambukiza kwani itawasaidia kuwaepusha na magonjwa hayo kwani yanaatahri kubwa katika maisha yao.


Aidha ametoa pongezi kwa shirikisho la vyama vya magonjwa yasiyo ya kuambukiza (TANCDA) pamoja   chama cha waandishi wanaopambana na magonjwa yasiyo ya kuambukiza (TJNCDF) kwa juhudi wanazo zifanya kwa kutoa elimu kwa wananchi kwani juhudi hizo ndizo zilizo changia kupatatika kwa tuzo hiyo hivyo waendelee kutoa elimu zaidi ili kuongeza nguvu kazi na hata kuimarisha uchumi wa Taifa na jamii kiujumla.  

Post a Comment

 
Top