0










Image result for ELIJAH MWANDUMBYA PICHA





Mamlaka ya mapato Tanzania(TRA) imewataka wafanyabiashara wote nchini kuhakikisha wananamba ya utambulisho ya mlipa kodi(TIN NAMBA) kwani kufanya hivyo itaongeza idadi ya walipa kodi na hata kupata taarifa sahihi za walipa kodi wanaostahili kukadiliwa na kutozwa kodi ili kuchangia kukua kwa pato la taifa.

Hayo yamesemwa na kamishina wa kodi za ndani kutoka mamlaka ya mapato Tanzania(TRA) Bw.ELIJAH MWANDUMBYA alipokuwa katika uzinduzi wa kampeni ya usajili wa walipakodi nchini kote iliyo fanyika Jijini DAR ES SALAAM yenye lengo la kuongeza wigo na idadi ya walipakodi.

Amesema kuwa ni muhimu  kwa walipa kodi  kuwa na namba hizo kwani zinawasaidia  kuepuka usumbufu pindi wanapolipa kodi na hata kuhisaidia  mamlaka hiyo kukusanya mapato kwa urahisi bila usumbufu wowote.
Pia MWANDUMBYA amesisitiza kuwa usajili wa TIN namba kwa walipa kodi ni bure na sio badala yake akatokea mtu akamdai mlipa kodi pesa kwaajili ya kupata namba hizo kwani hatakau ameenda kinyume na utaratibu.


AIDHA  ametoa wito kwa walipa kodi kuwa hakuna wakala yeyote aliyepewa jukumu la kusajili tin namba  hivyo basi  usajili utafanyika katika ofisi za mamlaka hiyo na katika vituo maalum ambavyo vitakuwa vimeteuliwa na kutangazwa kupitia vyombo vya habari mabalimbali hapa nchini.

Post a Comment

 
Top