0






 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjHqjYs06-Ji-gnJ6dnBuDkTx-RZ9DlEkFCCQTZM9vi8GuJOWxdvcLLHp_SphSZmRyK8QKLucHaAa533t2Tb79k18pKJuo3CY1AKR8r8-SdzO_haflAzSNTJGRg7q1frz8CvG6nTv6qB3s/s2560/%25255BUNSET%25255D.jpg






Shirika lisilo la kiserikali la Hakielimu limeiomba serikali kuwawekea mazingira mazuri wanafunzi wenye changamoto ya uoni mashuleni kwani kwakufanya hivyo itawasaidia wanafunzi hao kupata elimu iliyo bora na itakayo wasaidia katika maisha yao na hata kuondokana na utegemezi wa watu mbalimbali.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi mtendaji  wa shirika hilo  la HAKIELIMU JOHN KALAGE alipokuwa Jijini DAR ES SALAAM katika mkutano wa uzinduzi wa tathimini ya mafunzo na ushirikishwaji wa wanafunzi wenye changamoto ya uoni katika shule jumuishi hapa nchini.
Amesema kuwa mazingira mabovu kwa wanafunzi hao yamekuwa yakiwapa shida sana na hata muda mwingine kuwapelekea kushindwa kupata elimu iliyo bora ambayo ingewasaidia katika maisha yao na hata kuzifanya  familia zao  kupata maendeleo.
Pia ameeleza changamoto zinazowakabili wanafunzi wenye changamoto ya uoni mashuleni ikiwa ni pamoja na upungufu wa walimu wenye ujuzi wa kuwafundisha wanafunzi hao,kushindwa kutembea katika maeneo ya shule kutokana na miundombinu isiyo rafiki na kuwanyanyapaa wanafunzi wenye changamoto za uoni kutoka kwa baadhi ya walimu na hata kwa wanafunzi wenzao.
Aidha KALAGE ametoa wito kwa wadau mbalimbali,taasisi na mashirika kuendelea kushirikiana katika kutatua changamoto zinazo wakabili wanafunzi wenye changamoto ya uoni ili kuwafanya waweze kufika mbali kielimu na hata waweze kuondokana katika tatizo la utegemezi na waweze kujitegemea wenyewe.

Post a Comment

 
Top