0






 https://i2.wp.com/zanzibar24.co.tz/wp-content/uploads/2016/11/mkurugenzi-HESLB.jpg?fit=800%2C445







Waajiri nchini wametakiwa kuzingatia sheria  bodi ya mikopo ya wanafunzi wa  elimu ya juu hapa nchini(HESLB) ambayo inawataka kuwasilisha orodha ya majina ya waajiriwa wao ambao walikuwa ni wanufaika wa bodi hiyo pindi walipokuwa vyuoni ili kuiwezesha bodi hiyo kajua ni waajiriwa wangapi walikua wanufaika wa bodi hiyo.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu(HESLB) Bw.ABDULLAZAKI BADRU alipokuwa katika hafla iliyofanyika Jijini DAR ES SALAAM ya kuwatambua baadhi ya waajiri wanao timiza masharti ya bodi hiyo.

Amesema kuwa ni muhimu kila muajiri hapa nchini kuizingatia  sheria hiyo kwani imekuwa ikiisadia bodi hiyo kuongeza makusanyo kupitia waajiriwa  walikuwa ni wanufaika  na hatimaye kuwasaidi wanafunzi ambao bado  wapo vyuoni wanao hitaji mikopo kwa ajili ya kujiendeleza kielimu.

Pia ametoa pongezi  na kuzikabidhi ngao baadhi ya  kampuni na taasisi ambazo zimekuwa zikitimiza mashariti na kuzingatia sheria za bodi ya mikopo kwaiyo  amezitaka kuendelea na hali hiyo ili  kusaidia makusanyo ya pesa kupatikiana kwa urahisi bila matatizo yoyote kutoka waajiriwa wao.

Aidha nae Mkurugenzi Mtendaji wa urejeshaji wa mikopo kutoka katika bodi hiyo Bw.PHIDELIS JOSEPH amesema kuwa wataendelea kuwatembelea waajiri ili kubadilisha mawazo kwa lengo la kuongeza ufanisi na makusanyo na hata kuwasikia na kubadilisha mawazo ili hatimaye nchi iwe na waajiri wengi Zaidi wanaotimiza matwaka ya sheria ya bodi ya mikopo hapa nchini.

Post a Comment

 
Top