0

















Serikali kupitia mawakala wa huduma za ajira Tanzania (TaESA) imetoa wito kwa wananchi wenye taaluma na ujuzi katika sekta ya mafuta na gesi kujitokeza kwa wingi kujisajili kwa mawakala hao ili waweze kuingizwa kwenye kazidata  itakayo isaidia serikali kubaini adadi ya wananchi walio na sifa kwaajili ya kuwaunganisha katika mradi wa bomba la mafuta unaotaljiwa kuanza hivi karibuni.
Wito huo umetolewa  na kaimu mkurugenzi wa TaESA BONIFACE CHANDARUBA alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari Jijini DAR ES SALAAM kuhusu zoezi la utambuzi wa Watanzani wenye taaluma na ujuzi katika sekta ya mafuta na gesi.
Amesema kumekuwa na tatizo la ajira kwa wananchi  katika miradi mbalimbali inayoendelea hapa nchini hivyo serikali kupitia mradi wa bomba la  kusafirisha mafuta ghafi  linalotoka nchini Ungada hadi Tanzania imehamua kutoa fursa nyingi za ajira kwa wantanzani wenye taaaluma na ujuzi katika sekta hiyo kwa lengo la kuwanufaisha wao binafsi na taifa kiujumla.
 Pia ametoa wito kwa wanafunzi wanao maliza vyuo vikuu kuacha tabia ya kusubili ajira kutoka serikalini na badala yake wajiajili wenyewe kwani tatizo la ajira limekuwa kubwa hapa nchini na duniani kote hivyo nivyema wakalitambulia hilo na wakabadilika ili waweze kuondokana na tatizo hilo.
Aidha kwa upande mwingine nayo kampuni inayo jishugulisha na uuzaji wa mbolea hapa nchini  YARA LIMITED imahamu kuiunga mkono serikali katika kufanikisha  zoezi la uchumi wa viwanda linatimia kwaku  toa punguzo la bei  kwa mbolea wanazozalisha kwa lengo la kuwasaidia   wakulima  kuzalisha mazoa yakayokuwa bora na yenyetija kwa maendeleo yao na hata ya Taifa.

Post a Comment

 
Top